Mbeki awaunga mkono wapinzani wa Zuma
![Thabo Mbeki](https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/23F8/production/_95580290_mbekiafp.jpg)
PRETORIA,
Afrika Kusini
RAIS Mstaafu
nchini, Thabo Mbeki amewataka wabunge wa chama cha ANC kutenda yatakayowafaa
raia na sio kile kitakachofaidisha chama, wakati wa kujadili muswada wa
kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma, wiki ijayo.
Mwito wa huo
wa Mbeki (pichani), huenda ukawakera watu wanaomuunga mkono Zuma ambao wameapa kuupinga muswada
huo vikali bungeni, kulingana na tovuti ya IOL.
Upinzani
unadai kuwa Zuma ni fisadi na kuwa alimfuta kazi Pravin Gordhan kama Waziri wa Fedha,
licha ya kuwa Gordhan aliheshimika kwa kiasi kikubwa. Wanasema nia ya Zuma
ilikuwa kuchukua usukani katika wizara ya fedha.
Zuma amekuwa
akikanusha madai ya ufisadi, akisema kuwa yeye kufanya mabadiliko katika baraza
la mawaziri ni kwa manufaa ya raia
Kulingana na
tovuti hiyo, Mbeki alisema kuwa wabunge wanafaa kuwa sauti ya wananchi na wala
sio sauti ya vyama vya kisiasa. Anasema huu ni wakati wa Afrika Kusini kujua
ukweli kuhusu uhusiano wa kikatiba kati ya wananchi na viongozi wao wa kisiasa.
Mbeki ni
mwanachama wa ANC ambaye alijiuzulu kama rais baada ya kupoteza imani kwa chama
hicho kinachoongozwa na Zuma, mwaka wa 2008.
No comments