Zuma atakiwa kutohudhuria maziko ya mpinga ubaguzi
![https://businesstech.co.za/news/wp-content/uploads/2015/12/Jacob-Zuma-in-Germany.jpg](https://businesstech.co.za/news/wp-content/uploads/2015/12/Jacob-Zuma-in-Germany.jpg)
CAPE TOWN,
Afrika Kusini
RAIS Jacob
Zuma hatahudhuria mazishi ya mwanaharakati wa kuipinga Serikali ya Ubaguzi wa Rangi,
Ahmed Kathrada kwa ombi la familia yake.
Kathrada
alimtaka Zuma (pichani) ajiuzulu mwaka uliopita, kufuatia kashfa za ufisadi na kuilazimu
Serikali kuwakilishwa na Makamu wa Rais, Cyril Ramaphosa kwenye mazishi hayo.
Kathrada
mwenye umri wa miaka 87, aliaga dunia jana. Aliwahi kufungwa pamoja na Mandela
kwa kupinga utawala wa ubaguzi wa rangi.
Alitumikia
kifungo cha miaka 26 gerezani kabla ya kauchiliwa mwaka 1989. Baadaye alihudumu
kama mshauri wa rais wa zamani Nelson Mandela, kwenye Serikali ya kwanza
iliyochaguliwa kidemokrasia.
Zuma
alikuwa ameagiza bendera kupepea nusu mlingoti kufuatia kifo chake, na kuahirisha
mkutano wa mawaziri ili maofisa wapate kuhudhuria mazishi yake. Hata hivyo Zuma
hatadhuria mazishi wala ibada ya maombi ambayo itafanyika baadaye wiki hii,
kufuatia ombi la familia ya Kathrada.
Mke wa
Kathrada, Barbara Hogan anafahamika kuwa mkosoaji mkubwa wa Zuma. Awali, Kathrada
alimtaka Zuma ajiuzulu baada ya Mahakama ya Katiba nchini kuamua kuwa alikuwa
amekiuka Katiba kwa kukataa kulipa fedha ambazo zilitumiwa kukarabati makao
yake ya kibinafsi huko Nkandla.
Mwanaharati mpinga ubaguzi uliokuwa ukifanywa na utawala wa kikaburu nchini
Afrika Kusini, Ahmed Kathrada ambaye alifariki jana.
No comments