Header Ads

Rubani afariki ndege ikiwa safarini



Rubani afariki ndege ikiwa safarini Marekani
NEW MEXICO, Marekani
RUBANI wa ndege aina ya Boeing 737-800 mali ya kampuni ya American Airlines, William ‘Mike’ Grubbs amefariki dunia ghafla wakati ndege hiyo ikiwa kilometa chache kutua katika uwanja wa ndege wa Albuquerque.
Taarifa iliyotolewa na shirika hilo, ilieleza kuwa rubani huyo alifariki wakati ndege hiyo ilipokuwa ikielekea kutua katika uwanja huo wa Albuquerque kutoka ilikotokea Dallas.

Ndege hiyo aina ya Boeng 737-800, ilikuwa umbali wa kilometa tatu kabla ya kutua, wakati nahodha alipotangaza suala la dharura, kwa mujibu wa msemaji wa uwanja wa ndege wa Albuquerque
Ndege hiyo ilitua bila ya kisa chochote na hakuna aliyejeruhiwa. Mwaka 2015, rubani mwingine wa shirika hilo alifariki wakati wa safari kutoka Phoenix kuelekea Boston.
Ndege hiyo ilipelekwa na rubani mwenza kwa njia iliyo salama hadi uwanja wa Syracuse mjini New York. BBC

No comments

Powered by Blogger.