Header Ads

Mo Dewji aitembelea Juventus na kuahidi kuiunganisha na Simba SC




Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Mohamed Enterprises Limited (METL), Mohamed Dewji ‘Mo’ akiwa katika makao makuu ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia ‘Serie A’, Juventus FC alipotembelea hivi karibuni.
 


BILIONEA mwenye umri mdogo na mshindi wa tuzo ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Mohamed Dewji ‘Mo Dewji’ amefanya ziara katika makao makuu ya klabu ya mpira ya Juventus ya Italia na kuahidi kuwa atafanya kila awezalo kuiunganisha na Simba SC ya Tanzania.

Juventus ambao ndiyo mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia maarufu kama Serie A, imekuwa ikifanya vema katika misimu ya hivi karibuni katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya maarufu Uefa Champions League.
“Wiki hii nimekutana na Juventus FC, ambayo ni klabu yenye mafanikio zaidi Italia licha ya kuwepo kwa klabu nyinginezo kama vile AC Milan na Inter Milan”
“Ninatarajia kuitambulisha/kuiunganisha timu hiyo kwa uongozi wa Simba ili kujadili mambo kadhaa ya hapa na pale. Pia wameahidi kusaidia soka la Tanzania kwa kuendeleza soka la vijana” alisema Mo Dewji.
Chanzo: Azania Post

No comments

Powered by Blogger.