Header Ads

Dangote aapa kumtimua Wenger akiinunua Arsenal




LONDON- BILIONEA namba moja Afrika, Aliko Dangote amesema ndoto yake ya kuinunua Arsenal bado ipo na iwapo ataifanikisha, jambo la kwanza kulifanya klabuni hapo ni kumtimua kocha Arsene Wenger.
Dangote ambaye ni shabiki mkubwa wa timu hiyo, hakuwahi kuficha matakwa yake ya kuinunua klabu hiyo licha ya kuwa mmiliki Stan Kroenke kusisitiza hana mipango ya kuiuza.
Akizungumza na Bloomburg, Dangote alisema kwamba; “Kitu cha kwanza kukifanya nikishainunua Arsenal ni kubadilisha kocha. (Wenger) Amefanya kazi nzuri, lakini itakuwa nafasi nzuri kwa kocha mwingine kujaribu bahati yake.”
Dangote mwenye umri wa miaka 60, amesema kwa sasa ataendelea kupigania kuinunua timu hiyo baada ya kukamilisha ujenzi wa mtambo wa kusafisha mafuta wenye thamani ya pauni bilioni 8.5 (sh trilioni 24.6) Lagos nchini Nigeria.
Bilionea huyo mwenye utajiri wa pauni bilioni 10 (sh trilioni 29) kwa sasa, anadai kuwa Kroenke anayemiliki hisa asilimia 67 na Alisher Usmanov mwenye asilimia 30 ya hisa za Arsenal, endapo watapewa dau zuri basi watashawishika kuuza klabu hiyo.
“Wakipata dau lenye thamani kubwa, basi watashawishika kuiuza timu hiyo. Nitakapokamilisha ujenzi wa mtambo huo, nafikiri nitakuwa katika nafasi nzuri ya kufanya hivyo,” alisema Dangote.
Tofauti na matakwa ya Dangote kumtimua Wenger, kwa upande wake Kroenke anadai hana mpango wa kuiuza timu hiyo na anamuunga mkono kocha huyo na amemsisitiza kuipa mafanikio zaidi.
Daily Mail.

No comments

Powered by Blogger.