Qatar yaongezewa muda wa kutekeleza masharti

RIYADH- SAUDI ARABIA na nchi tatu za kiarabu zimeongeza
muda kwa Qatar, kutimiza masharti iliyopewa la sivyo iwekewe vikwazo zaidi
baada ya saa 48.
Tarehe ya
mwisho ya kuitaka Qatar kukubali masharti 13, ikiwemo ya kukifunga kituo cha Al
Jazeera ilimalizika jana. Taifa hilo la Ghuba, linasema kuwa litajibu kupitia
barua ambayo itawasilishwa kwa Kuwait leo Jumatatu.
Qatar
inakana madai kutoka kwa majirani zake kuwa inafadhili itikadi kali.
Waziri
wa Mambo ya Nje wa Qatar, Sheikh Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim Al-Thani
atasafiri kuenda Kuwait leo, kuwasilisha barua hiyo iliyotumwa kutoka kwa emir
wa Qatar kwenda kwa emir wa kuwait ambaye ndiye mpatanishi mkuu wa mzozo huo.
Siku ya
Jumamosi, Sheikh Jassim Al-Thani, alisema kuwa taifa hilo lilikataa masharti
hayo lakini liko tayari kwa mazungumzo.
Qatar
imekuwa chini na vikwazo vya kidiplomasia na kiuchumi kwa wiki kadhaa sasa, kutoka
Saudi Arabia, Misri, Falme za nchi za Kiarabu (UAE) na Bahrain.
No comments