Header Ads

Jeshi la Iraq laukomboa mji wa Mosul



Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi akiwapongeza baadhi ya makamanda waliofanikisha ushindi huo
BAGHDAD- WAZIRI Mkuu, Haider al-Abadi (pichani) ametembelea mji wa Mosul na kuwapongeza wanajeshi katika kile alichokiita ukombozi wa mji huo kutoka kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislamu (IS).

Hata hivyo, hakutangaza rasmi ushindi, akisema hilo litafanyika pindi vikundi vilivyobaki vitakapoondolewa. Mosul ndiyo sehemu ambayo kundi la IS lilipotangaza kuunda uongozi wake miaka mitatu iliyopita.
Sehemu kubwa ya mji huo imekuwa vifusi baada ya mapigano ya miezi tisa ya kuwaondoa wapiganaji hao.
Abadi ametembea katika barabara za mji wa Mosul na kuwapongeza wanajeshi.  Wakati huo huo, kumekuwa na sherehe pindi alipozuru eneo hilo.
Awali kulikuwa na taarifa za kuwepo mapigano, na moshi mzito ukionekana juu ya eneo ambao limekuwa ndio kitovu cha wapiganaji wa IS.
Kundi hilo la IS, bado linahodhi sehemu ya Magharibi na Kusini mwa Mosul na inaaminika litaendelea kufanya mashambulizi katika sehemu kubwa ya Iraq.
Islamic State waliuteka mji wa Mosul mnamo June 2014 na kuanzisha utawala wao. Vikosi vya Iraq, vikisaidiwa na mashambulizi ya anga kutoka Marekani, vimekuwa vikipambana kuirudisha Mosul tangu Oktoba 17 mwaka jana.
Maelfu ya raia wamekimbia huku wengine wakikosa pa kukimbilia wakati mapigano yakiendelea.
BBC

No comments

Powered by Blogger.