Header Ads

Watu 22 wafariki ajali ya basi India



Map of Bareilly
UTTAR PRADESH, India
TAKRIBAN watu 22 wamefariki dunia, baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugongana na lori mjini hapa.

Ajali hiyo ilitokea mapema leo, katika mji wa Bareilly uliopo kilometa 252 kutoka mji mkuu wa jimbo, Lucknow.
Ofisa wa cheo cha juu cha polisi mjini hapa, alisema waathiriwa wote kwenye ajali hiyo walikuwa na majeraha mabaya na hawatambuliwa mara moja.
Basi hilo la abiria lilishika moto kufuatia mgongano huo. Polisi wanamtafuta dereva wa lori lililohusika kwenye ajali.
Shirika la habari la AFP liliwanukuu polisi wakisema kuwa, milango ya basi iligoma kufunguka baada ya mlipuko hali iliyosababisha abiria kukwama ndani ya basi.
Watu wachache walifanakiwa kutoka nje kwa kuvunja madirisha ya basi.
India ina viwango vya ju zaidi vya ajali za barabarani duniani, ambapo ajali hutokea baada ya kila dakika nne.

No comments

Powered by Blogger.