Header Ads

IS wakiri kuhusika na shambulio la London



Image result for Islamic State


LONDON, Uingereza
KUNDI la kigaidi la Islamic State (Dola la Kiislamu) limekiri kuhusika kutekeleza shambulio la kigaidi lililosababisha watu saba na kujeruhi wengine 50 jijini hapa mwishoni mwa wiki.

Shambulio hilo lililotokea katika daraja la juu la London maarufu London Bridge, lilitokea baada ya magaidi hao kuwagonga watu kabla ya kuanza kuwachoma visu wengine.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi nchini, ilieleza kwamba watu watatu ambao walikuwa miongoni mwa washambuliaji hao waliuawa eneo la tukio na wengine wanaendelea kusakwa.
Aidha, Polisi wamebainisha kuwa wamekuwa wakifanya msako kwenye makazi manne mjini hapa, hadi usiku wa manane kama sehemu ya uchunguzi juu ya shambulio la Jumamosi ambapo watu saba waliuawa na wengine wapatao 50 walijeruhiwa.
Wachunguzi wanajaribu kubaini, ikiwa wanaume watatu walioendesha basi lao dogo na kuwagonga wapita njia kabla ya kuwachoma visu wengine wengi walipata msaada wowote.
Watu 11 wanashikiliwa kufuatia uvamizi wa polisi Mashariki mwa London. Kundi la Islamic State limesema lilihusika na shambulio hilo. Mwanamke mmoja raia wa Canada aliyeuawa katika shambulio hilo, ametajwa katika vyombo vya habari.
Taarifa ya familia yake imesema kuwa, alikuwa akifanya kazi katika hifadhi ya wasio kuwa na makazi kabla ya kuhamia Ulaya kuishi na mchumba wake. Watu 21 waliojeruhiwa katika shambulio hilo wako katika hali mahututi.





No comments

Powered by Blogger.