Header Ads

Terry kustaafu mwishoni mwa msimu huu



Terry amesema hakuna kilichosalia katika maisha yake uchezaji
LONDON, Uingereza
NAHODHA wa klabu ya Chelsea, John Terry amesema kuwa huenda akastaafu baada ya kuwasaidia mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kuilaza Watford kwa mabao 4-3 katika uwanja wa Stamford Bridge.

Terry (pichani) mwenye miaka 36 ambaye amefunga goli la kwanza katika mchezo huo, ataondoka mwishoni mwa msimu huu. Chelsea watakuwa wenyeji wa Sunderland siku ya Jumapili ikiwa ni mchezo wa mwisho kabisa kwa msimu huu.
Ameshinda vikombe vitatu vya EPL
Terry ameichezea Chelsea michezo 716 hii ikiwa ni tokea mwaka 1998. Ameisaidia Chelsea kushinda vikombe vitano vya FA, Vitatu vya Ligi ya EPL, kombe la mabingwa Ulaya mara moja na Europa ligi mara 1.


No comments

Powered by Blogger.