Header Ads

Marekani kujaribu kutungua makombora ya masafa marefu



Makombora ya Korea Kaskazini
Makombora ya Korea Kaskazini ambayo yamekuwa yakijaribiwa kila mara na kuleta hofu Marekani.
WASHINGTON DC, Marekani
IDARA ya Jeshi nchini, kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi bara lingine.

Maofisa wa Pentagon wanasema jaribio hilo litafanyika Jumatano, wiki ijayo. Hayo yanajiri, baada ya kuwepo kwa wasiwasi kuhusu uboreshaji wa miradi ya kinyuklia na makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini.
Mkuu wa shirika la ujasusi la Marekani, alisema iwapo miradi ya Korea Kaskazini ya kutengeneza makombora haitodhibitiwa, basi taifa hilo lina uwezo wa kutengeneza kombora lenye uwezo wa kufika Marekani.
Matamshi hayo yanaonesha wasiwasi wa Marekani kuhusu mpango wa Korea Kaskazini, wa kutengeza makombora ya mbali na mpango wake wa kinyuklia, ambayo taifa hilo inasema inahitaji kwa ulinzi wake.
Maofisa wa Serikali, walisema kuwa majaribio hayo yalipangwa mapema na kwamba haijibu kisa chochote. Pentagon ilitangaza jaribio hilo wakati ambapo Korea Kaskazini inatengeza kombora la masafa marefu.
Ni mara ya kwanza kwa Marekani kujaribu kuzuia kudungua kombora la masafa marefu ICBM. Marekani imekuwa ikitumia kifaa cha GMD kinachowekwa ardhini, kukabiliana na mashambulio ya mataifa kama vile Korea Kaskazini.
Kifaa hicho kina uwezo wa kudungua makombora mengine, lakini hawajajaribu kudungua makombora ya masafa marefu ambayo yanaweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine.
Huku maofisa wa Marekani wakiamini kwamba Korea Kaskazini ina miaka mingi ya kuweza kufanikiwa kutengeza kombora la masafa marefu la ICBM, lakini wanaamini taifa hilo limepiga hatua.


No comments

Powered by Blogger.