Aliyekuwa rais Korea Kusini Park Geun-hye 'kukamatwa'
SEOUL, Korea
Kusini
WAENDESHA Mashtaka
nchini, wamesema wataomba idhini ya kumkamata aliyekuwa rais ambaye aliondolewa
madarakani, Park Geun-hye, kwa mchango wake katika kashfa ya ulaji rushwa.
Park (pichani)
alipoteza kinga ya rais dhidi ya kufunguliwa mashtaka mapema mwezi huu na akaondolewa
rasmi madarakani baada ya Mahakama ya Katiba kudumisha uamuzi wa bunge wa
kumng'oa madarakani.
Park
anatuhumiwa kumruhusu rafiki yake wa karibu Choi Soon-sil kudai fedha kwa
lazima kutoka kwa kampuni kubwakubwa. Hata hivyo, Park alikanusha madai hayo na
kisha kuomba radhi kwa umma wiki iliyopita, kabla ya kuhojiwa na maofisa wa
mashtaka kwa saa 14.
Waendeshaji
mashtaka leo walisema kwamba ‘wameamua kwamba ni vema, kwa kufuata sheria na
maadili nchini, kuomba kibali cha kumkamata’.
Wanasema
ushahidi, ambao unapatikana katika diski za kompyuta huenda ukaharibiwa iwapo Park
hatakamatwa. Choi amefunguliwa mashtaka ya ulaji rushwa na tayari kesi dhidi
yake imeanza.
Park
aling'olewa vipi madarakani?
Park
aliondolewa madarakani kutokana na uhusiano wake wa karibu na Choi. Choi
anatuhumiwa kutumia uhusiano wake na rais huyo kushinikiza kampuni kutoa
mamilioni ya dola kama mchango kwa wakfu za kusaidia jamii ambazo alikuwa
anazisimamia.
Kaimu mkuu
wa kampuni kubwa ya vifaa vya kielektroniki ya Samsung, Lee Jae-yong,
alikamatwa kuhusiana na kashfa hiyo. Park, 65, anadaiwa kuhusika moja kwa moja
katika hili, na kwamba alimruhusu Choi uhuru wa kiwango kisichokubalika wa
kufikia nyaraka rasmi za serikali.
No comments