Trump atoa masharti mapya ya Visa
Hatua
hiyo inayahusisha mataifa yalio na Waislamu wengi kama vile Iran, Libya, Somalia,
Sudan, Syria na Yemen na tayari ujumbe umeshatumwa kwenye balozi zote za
mataifa hayo na balozi za Marekani katika mataifa hayo.
Masharti
hayo mapya yanayoanza kufanya kazi leo, yanaelezea mahusiano ya kifamilia kama
mzazi, mkeo ama mumeo, mtoto wa kiume ama wa kike ndiye anapaswa kuwapo nchini.
Masharti
hayo yanajiri baada ya Mahakama Kuu nchini, kuidhinisha kwa muda agizo la Rais
Trump ambalo lilikosolewa kuwa marufuku kwa Waislamu.
No comments