Header Ads

‘Marufuku kutuma sms kwa lugha za asili Kenya’



Image result for Kenya
NAIROBI- VYAMA vya Siasa nchini, vimeagizwa kusitisha mara moja au kufuta mipango yao ya kutuma jumbe fupi zilizoandikwa kwa lugha za asili kwa njia za simu kwenda kwa wananchi.


Jumbe hizo ambazo zimekuwa zikitumwa moja kwa moja kwa watu wengi, zimeelezwa kuwa ni zinachochea chuki na kusababisha kukithiri kwa ukabila na kurudisha nyuma juhudi za Serikali kukomesha ukabila.

Sheria hizo mpya ambazo zimezotelewa na Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA), pamoja na Tume ya Ushirikiano ya Taifa (NCIC) zinaeleza kwamba jumbe hizo zinapaswa kutumwa kwa lugha mbili tu ambazo ni Kiswahili na Kingereza.

Hayo yanajiri katika kipindi ambacho wanasiasa wameshikwa vikali na homa ya uchaguzi, ambao unatarajiwa kufanyika Agosti 8, mwaka huu ili kuwazuia wanasiasa hao kutumia majukwaa yao kwenye mitandao ya kijamii na simu kueneza chuki.

Chini ya sheria hizo kali, wakala wa kusimamia maudhui wamewaandikia barua rasmi za kuzitaka kampuni simu kubainisha chama au vyama vinavyosambaza jumbe za chuki na zilizoandikwa kwa lugha za asili.

No comments

Powered by Blogger.