Kadinali matatani kwa unyanyasaji wa kingono
Kadinali
Pell (pichani) amekanusha makosa hayo ambayo yanasemekana kufanyika miaka ya 1970. Anatarajiwa
kufikishwa mbele ya mahakama mjini hapa Julai mwaka huu.
Licha
ya mashtaka hayo dhidi ya mtumishi wao, wawakilishi wa kanisa hilo hawajatoa
tamko lolote juu ya suala hilo licha ya BBC kutoa ombi la kuwataka kufanya
hivyo.
Idara
ya Polisi, iliamua kuchukua hatua ya kumfungulia mashtaka Kadinali Pell, baada
ya kupata ushauri kutoka kwa viongozi wa mashtaka mwezi uliopita.
Naibu
Kamishna wa polisi, amesema mchakato wa kumfungulia mashtaka kadinali huyo hauna
tofauti yoyote na uchunguzi wowote.
Kadinali
Pell ni Mwekahazina wa Vatican na Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini. Maofisa wa polisi wa jimbo la Victoria,
wamesema mashtaka hayo yanatokana na madai ya ‘kihistoria’.
“Madai
hayo yalitolewa na zaidi ya mtu mmoja” alisema naibu kamishna wa polisi, Shane
Patton. Kadinali Pell ambaye makao yake makuu yako Vatican, amekana madai hayo.
Akiwa
mwekahazina wa Vatican, Kadinali Pell anatambulika kuwa ofisa wa tatu mkuu
katika kanisa hilo.
Katika
taarifa iliyotolewa na kanisa hilo, Kadinali Pell atarudi nchini haraka
iwezekanavyo, ili kujisafishia jina lake kufuatia ushauri ulioungwa mkono na
madktari wake ambao pia watamshauri kuhusu mipango yake ya kusafiri.
Alisema
kuwa yuko tayari kufika mahakamani na atajitetea mashtaka yanayomkabili.
Kadinali
huyo siyo mkuu wa kanisa hilo nchini, bali pia ni miongoni mwa viongozi wakuu
walio na hadhi ya juu katika ulimwengu wa kanisa hilo.
Katika
kipindi cha miongo miwili, amekuwa amekuwa katika mstari wa mbele katika
mjadala wa kanisa hilo kuhusu masuala tata kama vile lile la wapenzi wa jinsia
moija, ukimwi na utafiti wa seli.
Pia
amehusika katika kutoa majibu ya kanisa hilo kuhusiana na madai ya unyanyasaji
wa kingono nchini.
No comments