Header Ads

Italia yatishia kuzuia wahamiaji kuingia pwani zake



Moja ya meli yenye wahamiaji ikiingia Italia
ROME- SERIKALI imetishia kuzuia meli za mataifa mengine kuwashusha wahamiaji katika bandari zake.

Mwakilishi wa taifa hilo katika jumuiya ya mataifa ya bara Ulaya, Maurizio Massari, ameonya kuwa idadi ya wahamiaji wanaovuka bahari ya Mediterranea kutoka Afrika Kaskazini inazidi kuongezeka.
Karibu watu 10,000 wameripotiwa kujaribu safari hiyo siku chache zilizopita.
Awali kamishna wa masuala ya uhamiaji ya EU, Dimitris Avramopoulos, alisema mataifa yote wanachama wa EU yalikuwa na jukumu la kibinadamu la kuokoa maisha na kwamba hayangeweza kuachia jukumi hilo mataifa machache kakabiliana na suala hilo.
Mataifa 28 wanachama wa jumuiya hiyo wametoa chini ya nusu ya Euro milioni 200 waliyoahidi kukabiliana na wahamiaji kutoka Afrika, hususan Libya ambako ndiko kituo kikuu cha mwanzo wa safari.

No comments

Powered by Blogger.