Header Ads

Helikopta iliyoshambulia mahakama Venezuela yapatikana



Ilikutwa kajika jimbo Vagas pwani kaskazini
CARACAS- VIKOSI vya usalama nchini, vimefanikiwa kuipata helikopta iliyotumiwa na ofisa muasi wa polisi kupaa juu ya majumba ya Serikali mjini hapa na kushambulia jengo la Mahakama ya Juu kwa kuangusha guruneti na kupiga risasi jana.

Makamu wa Rais, Tareck El Aissami amesema helikopta hiyo ilipatikana karibu na karibu na jimbo la Vagas lililopo pwani ya Kaskazini mwa nchi, kilometa 45 kutoka hapa Caracas.
Alitoa picha zinazoonesha helikopta hiyo katika maeneo ya milima ikisafisha maeneo yaliyozungukwa na migomba ya ndizi.
Kufikia sasa hakuna dalili yoyote ya kupatikana kwa rubani wa helikopta hiyo, Oscar Lopez, ambaye alikuwa ni ofisa polisi aliyeamua kuasi na kutekeleza kitendo kilichodaiwa na Serikali kama kisa cha kigaidi.


No comments

Powered by Blogger.